Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna    
Risala yetu: Kudhihirisha miujiza ya kisayansi Na kuihakiki na kuichapisha.

Lugha

Muhtasari Wa Utafiti Kuhusu Bodi Wasiliana Nasi  

Ni nini miujiza ya kisayansi?

     Miujiza ya kisayansi ni aina kati ya aina za miujiza ya Qurani na inakusanya:

·        Miujiza ya bayana na lugha.

·        Miujiza ya kihabari (kihistoria).     

·        Miujiza ya kisheria.

·        Miujiza ya kisayansi.

     

      Na miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna. Ni aina ya tafsri ya kisayansi, nako ni kuzielezea Qurani Tukufu na Sunna za Mtume kwa maana ya wazi kabisa katika kifungu kwa mujibu wa misingi ya tafsri ya kisayansi kwa ukweli thabiti wa kisayansi, ambao umethibitika kutokuwepo uwezo wa kufahamika kwake kwa njia za binadamu katika wakati wa Mtume (S.A.W). Haya ndiyo yaliyodhirisha ukweli wa Mtume Muhammad (S.A.W) kwa aliyoeleza kuhusu Mola wake aliyetakasika.

KUASISIWA KWA BODI NA KUENDELEZWA KWAKE.

 

·        Bodi ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna imeasisiwa mwaka 1404 Hijria kwa uamuzi wa baraza kuu la dunia la misikiti katika mkutano wake wa tisa.

·        Katika mwaka 1406 Hijria, baraza kuu la dunia la misikiti limepitisha kuanzishwa kwa bodi miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna na katibu wake mkuu wa kwanza alikuwa ni mtukufu Sheikh Abdel Majid Al-Zindani. Bodi hiyo ikachukua makao makuu yake kwenye Jumuiya ya ulimwengu wa Kiislamu Makkah Al Mukaramah, na ikawa na matawi yake mengine ndani na nje ya Saudi Arabia kwa ajili ya kufikia malengo yake.

·        Katika mwaka 1423, Hijria baraza la uasisi la Jumuiya ya ulimwengu wa kiislamu katika mkutano wake wa thelathini na saba, limeamua kuendeleza bodi  na ikawa inaitwa: “ Bodi ya kumataifa ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna”. Nayo ni moja ya bodi za Jumuiya ya ulimwengu wa Kiislamu yenye haiba ya kujitegemea kikanuni na yenye kufanyika na:

·        Halmashauri kuu, baraza la uongozi, kamati tendaji, katibu mkuu.

·        Mheshimiwa Dk. Abdullah Al-Muslih akawa katibu mkuu wa bodi mwaka 1423 Hijria hadi hivi sasa.

  

MALENGO  YA  BODI

 Bodi inafanya kazi kuyafikia malengo yafuatayo:

 

·        Kuweka misingi na sheria ambazo zinapanga jitihada katika kubainisha miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.

·        Kufichua maana za ndani kabisa za aya katika kitabu cha Mwenyezi Mungu na hadithi tukufu za Mtume zinazohusiana na sayansi ya dunia katika mwangaza wa misingi ya tafsiri na pande za maana ya kilugha na makusudio ya sheria ya Kiislamu bila ya kujikalifisha.

·        Kuunganisha sayansi za kidunia na ukweli wa kiimani na kuingiza yaliyomo kwenye tafiti zilizokubalika katika mitaala ya mafunzo katika taasisi na viwango mbali mbali.

·        Kuchangia katika kuandaa wataalamu na watafiti kwa ajili ya kudurusu masuala ya kisayansi na ukweli wa kidunia katika mwangaza wa yaliyothibiti katika Qurani na Sunna.

·        Kuzielekeza programu za miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna ili iwe ni njia kati ya njia za ulinganio.

·        Kuratibu juhudi zinazotolewa ulimwenguni katika uwanja wa miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna na kushirikiana na taasisi na vituo vyenye kuhusika.

Bodi inatumia njia ambazo zinakubaliana na hukumu za sheria ya Kiislamu: Kati ya hizo ni:

 

1.     Kuweka vipimo vya kutathmini tafiti zinazohusiana na miujiza ya kisayansi katika Qurani  na Sunna.

2.     Kuzidurusu aya za Qurani na hadithi za Mtume zinazohusu masuala ya miujiza ya kisayansi.

3.     Kudurusu tafiti za miujiza ya kisayansi nakuziangalia kwa kina kwa upande wa kisheria na kidunia na kuruhusu yanayofaa kati yake.

4.     Kuhamasisha tafiti za mtu peke yake na za makundi ya watu katika uwanja wa miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.

5.     Kuratibu juhudi za watafiti wanaofanyakazi katika uwanja wa miujiza ya kisayansi.

6.      Kufuatilizia yanayofikiwa na wataalamu katika nyanja za kidunia, wanayoandika na wanayochapisha  kuhusu masuala ya kisayansi yanayoshikamana na Qurani na Sunna, durusu zake na tathmini zake.

7.     Kuimarisha uhusiano na wanaohusika na elimu za kiislamu na kidunia kati ya waislamu na wasiokuwa waislamu.

8.     Kuwasiliana na bodi zinazohusika na elimu za kiislamu na kidunia na kubadilishana maelezo.

9.     Kutoa vitabu na majarida yenye shime ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna na kuvisambaza kwa wenye shime na wenye kupenda ulimwenguni.

10. Kuitisha mikutano, semina na vikao vya tafiti zinazohusika na  miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna, na kuzichapisha tafiti zake na kushirikim katika mikutano na semina nyengine zenye kuhusika.

11. Kuchapisha tafiti zilizopitishwa kwa inayolingana na viwango vya watu vya kielimu na kitamaduni na kuzifasiri kwa lugha mbali mbali.

12. Kuwapatia walinganiaji na waenezi ulimwenguni – mtu mmoja mmoja na taasisi – kuwapatia tafiti zilizopitishwa kati ya hizo, kila moja katika uwanja wake.

13. Kushirikiana na taasisi za kisayansi na bodi za kisayansi zinazohusika na kufanya vikao na mikutano baina ya wenye kufanyakazi katika masuala ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.

14. Kujitahidi kwa wahusika, wa elimu binafsi na ya serikali, katika taasisi za kielimu na mashirika ya kiislamu yenye shime na sayansi na utamaduni, kuziingiza tafiti zilizopitishwa na bodi katika jumla ya mitaala ya kielimu katika awamu tofauti za masomo zinazofaa.

15. Kuvihimiza vyu vikuu kutoa nafasi na kuhamasisha usajili katika miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.masomo ya juu na kutoa nfasi za masomo katika uwanja wa

 
 

 

 

 

 

Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna   (1428-2007)