Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna    
Risala yetu: Kudhihirisha miujiza ya kisayansi Na kuihakiki na kuichapisha.

Lugha

Ukurasa Kuu Muhtasari Wa Utafiti Kuhusu Bodi Wasiliana Nasi  

SIFA ZA BAHARI ZENYE KINA KIREFU

Mwenyezi Mungu Amesema, “Au (amali zao zile mbaya) ni kama giza katika bahari yenye maji mengi, inayofunikwa na mawimbi juu ya mawimbi; na juu yake kuna mawingu; giza hili juu ya hili; anapoutoa mkono wake anakaribia asiuone (kwa kiza kilivyoshtadi) na ambaye Mwenyezi Mungu Hakumjaalia nuru, hawi na nuru.”

UHAKIKA WA KISAYANSI:

          Insaiklopedia la Uingereza linasema kuwa mara nyingi bahari na bahari zenye kina kirefu huwa ni zenye kufunikwa na kiwingu kizito chenye kuzuia kiasi kikubwa cha mwanga wa jua kama inavyodhihiri katika picha nyingi za satalaiti. Mawingu hayo huakisi kiasi kikubwa cha mionzi ya jua na hukinga kiasi kikubwa cha mwanga wake. Ama mwanga uliobaki, basi maji huakisi sehemu yake na kufyonza sehemu nyengine ambayo inapingana kwa wima pamoja na kuzidi kwa kina cha maji. Hufanyika ngazi za kiza ndani ya bahari hizo hadi kina cha meta mia mbili, na kiza huzidi baada ya kina cha meta 1000, kwani haiwezekani kuona kabisa. Diski ya Secchi (The Secchi disk) ni chombo cha kwanza kutumika kwa ajili ya kupima kina cha kupenya mwangaza katika maji ya bahari.

         Wataalamu wameweza kuangalia samaki katika bahari kubwa kwenye kina baina ya (meta 600 – 2700) wanaotumia  viungo vyenye kutoa mwanga ili kuona katika kiza na kukamata viwindo vyao.

         Imegunduliwa sayansi mpya ya bahari mwishoni mwa karne ya kumi na tisa baada ya kutumia mbinu za upigaji picha zilizoendelezwa katika miaka ya thelathini ya karne ya ishirini, ambapo zimetumika seli za mwanga wa umeme ambazo zimegundua kuwepo kwa mawimbi makubwa katika bahari zenye kina kirefu. Insaiklopedia la Uingereza linasema kuwa hali ya mawimbi ya ndani yaliyopo katika vina virefu vya bahari, hayakujulikana na binadamu isipokuwa kabla ya miaka mia moja tu, ambayo hutokana na kutandawaa kwa mwanya baina ya tabaka mbili za maji tofauti kwa upande wa eneo, shinikizo, joto, kupwa na kujaa na athari za upepo. Upeo wenye kutenganisha unafanyika baina ya maeneo tofauti kwenye eneo la mshuko mkuu wa joto ambapo maji ya upeo wenye umotomoto hutenganika na maji ya kina cha ubaridi.

         Mawimbi haya yanayofanyika kwenye usawa huo unaotenganisha baina ya tabaka mbili tofauti za maji katika eneo, chumvi na joto, yanafanana na mawimbi ya usawa wa juu, lakini haiwezekani kuyaona kirahisi toka juu ya maji. Zoezi la kufanyika kwake linachukua kiasi kikubwa cha nishati ambayo ingewezekana kutumika katika kusukumia meli mbele. Tunakuta baadhi ya meli zenye kupita katika maji hayo, mara moja hupoteza nguvu yake ya kusonga mbele. Huingia kwenye kile kinachoitwa hali ya maji yaliyotuama ambayo fadhila za kufasiriwa na kudurusiwa kwake zinarejea kwa Dk. Van W. Ekman wa Sweden mwanzoni mwa karne ya ishirini.

UPANDE WA MIUJIZA:

          Zamani binadamu alikuwa akiamini mambo mengi ya kijinga kuhusu bahari na bahari kubwa. Mabaharia wakati huo hawakuwa na maarifa ya kweli ya kisayansi kuhusu hali zilizoko katika vina virefu vya bahari. Maelezo kuhusu pepo za bahari yalikuwa haba.

         Na haya ndiyo yaliyozuia mambo ya kijinga kuijua bahari iliyotuama isiyoweza kupitiwa na meli. Warumi wa kale waliamini kuwepo kwa samaki wenye kufyonza wenye athari za kichawi katika kusimamisha mwendo wa meli. Licha ya kuwa watu wa kale walikuwa wakijua upepo ndio wenye kuathiri mawimbi ya juu, lakini ilikuwa ni vigumu kujua chochote kuhusu mwendo wa mawimbi ya ndani katika bahari yenye kina kirefu. Historia ya sayansi inabainisha kuwa durusu zisizokatika za sayansi ya bahari na vina vyake, hazikuanza isipokuwa mwanzoni mwa karne ya ishirini wakati vilipogunduliwa vyombo vinavyofaa vya durusu nyeti kama hizo. Sayansi mpya ya bahari, imeweza kugundua katika nusu ya pili ya karne siri za kushangaza katika vina vya bahari na bahari kubwa kwa kugundua hali mbili: Kiza cha bahari yenye kina kirefu, na mwendo wa mawimbi ya ndani. Aya tukufu imeashiria hali hizi mbili.

         Aya tukufu imeashiria hali ya kiza katika bahari zenye kina kirefu kwa kuielezea kuwa ni bahari yenye maji mengi, nayo ni bahari yenye kina kirefu. Na kiza katika bahari hizo ni kiza chenye kupanda kidogo kidogo. Wanafasiri wamesema: Makusudio ya viza hivyo ni kiza cha mawingu, kiza cha mawimbi na kiza cha bahari. Anayekuwa katika viza hivyo, hawezi kuona chochote. Mawingu mazito yenye kuziba bahari hizo, huzuia kiasi cha mwangaza wa jua, na  bahari kwa  mawimbi yake ya juu, huzuia sehemu nyengine ya mwangaza huo. Kisha maji hufyonza rangi za jua moja baada ya nyengine hadi rangi hizo hupotea kabisa. Kisha inakuja zamu ya mawimbi ya ndani yanayogeuza vina virefu kuwa ni kiza totoro hata binadamu akitoa mkono wake hawezi kuuona. Yamekuja maelezo ya kiza juu ya kiza kuelezea hali katika bahari kwa uwazi kabisa. Pia samaki katika vina hivyo virefu, hawana macho bali wana viungo vyenye mwangaza  ambavyo Mwenyezi Mungu Ameviumba katika miili yao kuwaangazia njia yao. Na haya ndiyo maneno Yake Mwenyezi Mungu, “ Na ambaye Mwenyezi Mungu hakumjaalia nuru, hawi na nuru.”

          Aya pia imeashiria mwendo wa mawimbi ya ndani katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu, “ Katika bahari yenye maji mengi, inayofunikwa na mawimbi juu ya mawimbi.” Maana yake ni kuwa mawimbi yanafunika bahari yenye maji mengi. Na haya ndiyo yaliyothibitishwa na wataalamu wa bahari pale waliposema kuwa bahari yenye maji mengi na yenye kina kirefu, ni tofauti na bahari ya juu, kwani ndani yake mna mawimbi katika eneo lenye kutenganisha baina ya bahari ya juu na bahari yenye kina kirefu, ni tofauti na mawimbi ya juu, jambo ambalo halikujulikana isipokuwa tokea miaka mia moja tu.

         Ukweli huu wa kisayansi wa kushangaza umetajwa na Qurani Tukufu tokea karne kumi na nne. Ni nani aliyemfahamisha Muhammad (S.A.W)? Ni Mwenyezi Mungu ulio juu utajo Wake.

 

Tafsili: Kiarabu   

              Kiingereza   Kifaransa     Kijerumani      Kispani      Kituruki       Kiurdu    Kifarsi     Kihausa
 
 

Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna   (1428-2007)