|
UHAKIKA WA KISAYANSI:
Vitabu vya historia vinaelezea kutokea kwa vita baina ya
malaka mbili ya Waajemi na utawala wa Bezante, nayo ni
sehemu ya mashariki ya utwala wa Warumi, katika eneo la
baina ya Azriat na Basry karibu na bahari maiti (Dead
Sea) ambapo Waajemi walipata ushindi mkubwa mno
kuwashinda Warumi na hiyo ilikuwa katika mwaka 619 AD.
Warumi wa Bezante
wakapata hasara kubwa mno katika vita hivyo na wote
walioishi wakati huo wakategemea kuwa wataangamia kabisa
na utawala wao. Lakini yalitokea yale ambayo
hayakutegemewa. Katika mwezi wa Desemba mwaka 627AD,
vilitokea vita vya mwisho baina ya Wabezante na utawala
wa Waajemi katika eneo la Nineveh. Warumi wakawashinda
Waajemi. Na baada ya miezi michache, Waajemi walitaka
kutia saini mkataba na Wabezante uliowalazimisha
kuzirejesha ardhi walizozichukua kwao.
Picha za kijiografia za
maeneo ya mabonde ya ardhi duniani zinaonyesha kuwa eneo
lililo chini kabisa juu ya uso wa ardhi ni lile eneo
lililo karibu na bahari maiti (Dead Sea) nchini
Palestina, kwani liko chini ya usawa wa bahari kwa kina
cha meta 395. Yamethibitishwa hayo na picha na vipimo
vya setalaiti. |
|
UPANDE WA MIUJIZA:
Kuna pande mbili za
miujiza katika aya hizi tukufu. Kwanza ni kule Qurani
tukufu kuelezea ushindi wa Warumi kuwashinda Waajemi
baada ya kushindwa kwao vibaya sana, baada ya miaka
kadhaa. Na miaka kadhaa maana yake ni miaka baina ya
mitano na saba, au baina ya mwaka mmoja na miaka tisa,
kama wasemavyo wataalamu wa lugha. Yametimia
yaliyoahidiwa na Qurani tukufu baada ya miaka saba,
kwani vilitokea vita vyengine baina ya Waajemi na Warumi
mwaka 627AD na Warumi wakashinda. Haya yamekwenda
sambamba na ushindi wa Waislamu kwa washirikina wa
Qureish katika vita vikubwa vya Badr. Ushindi huo
ulionekana mgumu katika macho ya Waarabu washirikina kwa
kiasi ambacho wakaanza kuwakejeli kutokana na aya hizi
za Qurani na wakaweka rehani kwa Waislamu ikiwa
utapatikana ushindi huo unaodaiwa. Yakapotea matumaini
yao na ukatimia muujiza wa Qurani Tukufu wakati watu
walipotoa mapema habari za ushindi wa Warumi.
Upande wa pili wa miujiza
katika aya hizi tukufu ni kuwa umetokea ukweli wa
kijiografia uliokuwa haujulikani na yeyote katika wakati
huo. Aya zimeelezea kuwa Warumi watashindwa vita na
Waajemi kwenye eneo lililo chini kabisa katika ardhi.
Neno (Adna) katika Lugha ya Kiarabu lina maana mbili,
karibu na chini zaidi. Kwa upande mmoja ni eneo la
karibu zaidi na Bara Arabu, na kwa upande mwengine ni
eneo lililo chini kabisa juu ya uso wa ardhi, kwani liko
chini ya usawa wa ufukwe wa bahari kwa futi 1312 (kiasi
cha meta 400). Nalo ni eneo lililo chini kabisa
kurekodiwa na setelaiti juu ya eneo kavu. Pia yameelezwa
hayo na kamusi ya Uingereza. Na ukweli wa kihistoria
unahakikisha kuwa vita vimetokea katika maeneo ya dunia
yaliyo chini zaidi ya bonde la Bahari Maiti (Dead Sea)
ambayo yasingeweza kupimwa katika hali ya kutokuwepo kwa
teknolojia ya vipimo ya kisasa. Kwa hiyo ilikuwa
haiwezekani kwa mtu yeyote wakati huo kujua kuwa eneo
hilo ni eneo lililo chini kabisa duniani. Je, hivyo hii
sio dalili ya kwamba Qurani ni wahyi na inatoka kwa
Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu Mtukufu Amesema, “
Sema: Namshukuru Mwenyezi Mungu, Atakuonyesheni aya zake
na mtazijua.” |