|
|
|
KUUMWA KWA
KIWILIWILI |
|
Mtume (S.A.W) amesema, “ Mfano
wa Waumini katika kupendana kwao, kuhurumiana kwao, na
kuoneana imani kwao, ni sawa na kiwiliwili. Kikiumwa
kiungo kimoja, basi mwili mzima hukesha na kupata homa.”
(Imepokelewa na Bukhari na Muslim
na wengineo). |
|
UHAKIKA WA KISAYANSI:
Tafiti pevu na za
kuendelea bila ya kusita za kisayansi, zimethibitisha
ukweli wa kushangaza kuhusu maingiliano ya mwili wa
binaadamu wakati wa kukabiliana na hatari kama vile
kujeruhiwa au kuumwa. Imegunduliwa mistari ya kinga na
kuitikia kikazi ambako kunatokea kwenye mwili wakati wa
kiungo kati ya viungo vyake kuumwa au kujeruhiwa.
Mshituko huo unakwenda sambamba na kiwango cha tabu ya
kiungo kwa mwendo wa uwiano. Kwa kadri ya maumivu ya
kiungo yanavyokuwa, ndivyo inavyokuwa nguvu ya mwili na
kazi zake kwa ajili ya kuzuia kukomaa kwa maradhi na
kufikia kupona kamili. Katika hali ya kujeruhiwa kwa
kiungo, kwa mfano vituo vya ubongo huita (Tezi
pituitari) ili itoe homoni
inayotoa wito kwa (Tezi endokirini)
ambazo hutoa mada za
motisha na kuvitolea wito viungo vyote kutekeleza kazi
zao kukiokoa kiungo chenye kuumwa. Mwili huelekeza
nguvu zake zote kukihudumia kiungo kinachouma. Moyo kwa
mfano, huharakisha mapigo kwa uharaka wa mzunguko wa
damu katika wakati ambao mishipa ya damu inajishika na
sehemu za mwili zilizochoka na hupanuka mishipa ya damu
iliyo jirani na kiungo kinachoumwa ili kukipatia
mahitaji yake ya nishati, oksijeni, kiuavijasumu, homoni
na baadhi ya asidi katika hali yake ya kuumwa kwa maana
ya kubomoka na kuporomoka. Huanza kwa kubomoka kwa
hazina ya mafuta ili chenyewe kiweze kukipa kiungo
kinachoumwa mahitaji yake hadi kiweze kuyadhibiti
maradhi na tishu ziweze kushikamana. Kisha baada ya
hapo, mwili unarejea kujijenga wenyewe. Ishara
zinazotoka kwenye jeraha ni sawa na malalamiko na kuomba
msaada wa kweli zenye kupelekea kuchukuliwa. Huchipuka
mapigo ya nava toka sehemu inayoumwa kuelekea kwenye
ubongo ambako kuna vituo vya hisia, uthibiti unatokea
wenyewe na kutoa mada za kemikali pamoja na tone la
kwanza la damu lenye kumwaika mshipa wenye kukatika.
Huitikia viungo vya mwili wote kila kimoja kwa mujibu wa
kazi yake, na matokeo ni kuelekeza nishati ya mwili wa
binadamu na kazi za viungo vyake kwa ajili ya kuhudumia
kiungo hicho kinachoumwa. |
|
UPANDE WA MIUJIZA:
Mantiki ya hadithi
ndiyo yenye kutokea kitiba. Sehemu za mwili huitana
zenyewe kwa zenyewe na kwa maana zote za kuitana. Mtume
(S.A.W) anatoa habari kuhusu yanayopaswa kuwa na umma wa
Kiislamu kuhusiana na kupendana, kuhurumiana na kuoneana
imani kwa kutoa mfano wa mwili mmoja wakati kiungo
kimoja kinapougua. Amebainisha kuwa vinaitana vyote kwa
ajili ya kiungo hicho. Ametoa habari juu ya ukweli wa
yanayotokea ndani ya mwili wa binadamu, kwani jicho
lisingeweza kuuona kwa kutumia maneno yenye kuuelezea
ukweli wa yanayotokea kwa maana zote zilizokuja katika
lugha kwa mtindo wa kufanananisha ambao unaleta maana
katika akili. Ni jambo la kushangaza kwa madaktari
kutumia majina ya chombo cha nava ambacho
kinachanganyika katika hali ya mwili kupatwa na hatari
na maradhi na kuelezea ukweli wa kinachofanywa na mfumo
huo na chombo hicho. Na tafsri yake ya neno ikawa ni:
kupendana, kuhurumiana na kuoneana imani, nayo ndiyo
hayo hayo yaliyosemwa na Mtume (S.A.W) katika hadithi.
Ametakasika Mwenyezi Mungu Aliyemtuma Mtume wake kwa
uongofu na dini ya haki ili kuidhihirisha kwa dini zote
na akampa aya za wazi na jumla ya maneno. |
|
 |
|
Seli zinaitikia wito wa sehemu inayoumwa nahushambulia
gesi zinazoingia na kuziangamiza kasha kuzitoa .Miujiza
ya kitiba katika Sunna tohara: mwili unatoa wito kwa
kujeruhiwa na maradhi. |
|
Tafsili:
Kiarabu
 |
|
Kiingereza
Kifaransa Kijerumani Kispani Kituruki
Kiurdu
Kifarsi Kihausa |
|
|