Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna    
Risala yetu: Kudhihirisha miujiza ya kisayansi Na kuihakiki na kuichapisha.

Lugha

Ukurasa Kuu Muhtasari Wa Utafiti Kuhusu Bodi Wasiliana Nasi  

SAYANSI  YA  UCHUNGUZI  WA  MWILI  INAAINISHA VITENGANISHI VYA MWILI

    Imehadithiwa na Imam Muslim toka kwa Abdullah bin Furukh, amemsikia Aisha akisema kuwa Mtume (S.A.W) amesema, “Kila mtu ameumbwa kutokana na watoto wa Adam kwa viungo mia tatu na sitini. Anayemkabiri Mwenyezi Mungu, akamhimidi Mwenyezi Mungu, akasema La ilaha ila Allah, akamuomba maghfira Mwenyezi Mungu, akaondosha jiwe kwenye njia ya watu au mwiba au mfupa kwenye njia ya watu, na akaamrisha mema au akakataza mabaya kwa viungo hivyo mia tatu na sitini, basi anakwenda siku hiyo hali ya kuwa ameiokoa nafsi yake na moto”.

 Imepokelewa na Imam Ahmad kwa kutegemea Abdulla bin Baraidah amesema: Nimemsikia Abi Buraidah anasema: Nimemsikia Mtume (S.A.W) anasema “ Katika mwili wa binadamu, kuna viungo mia tatu na sitini, ni juu yake kutoa sadaka kwa kila kiungo kati ya hivyo. Wakasema: Ni nani anayeweza hayo, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: Ni kohozi katika msikiti analolifukia, au kitu anachokiondosha kwenye njia. Na asipoweza kufanya hivyo, basi ni juu yake kusali rakaa mbili za Adh dhuha, zitatosheleza.”

UKWELI WA KISAYANSI:

          Vitenganishi vya mwili, ni makutano baina ya mifupa yoyote miwili au mfupa na mfupa laini au mifupa miwili laini kwenye sehemu ya mwili wa binadamu muda wa kudumu kuna kitenganishi baina yao.

IDADI YA VITENGANISHI KWA MUJIBU WA KANUNI ZILIZOWEKWA :

1. Vitenganishi vya fuvu

86

2.Vitenganishi vya koo

6

3. Vitenganishi vya mrija wa kifua

66

4. Vitenganishi vya uti wa mgongo na hodhi

76

5. Vitenganishi vya viungo vya juu                              2 (32)

64

6. Vitenganishi vya viungo vya chini                           2 (31)

62

                                                                                                                          JUMLA

360

UPANDE WA MIUJIZA:

          Mtume (S.A.W) ameelezea idadi ya vitenganishi vilivyopo katika mwili wa binadamu kuwa ni mia tatu na sitini katika wakati ambao ni vigumu kujua idadi hiyo kwa usawa kabisa. Vitenganishi vingi kati ya hivyo ni nyeti na vipo katika sehemu ambazo ni vigumu kuviainisha kwa kuviangalia kwa macho matupu. Na wala havikuainishwa kwa uwazi kabisa isipokuwa baada ya kuendelea kwa sayansi ya uchunguzi wa mwili na sayansi ya tishu na vitenganishi vya mwili, navyo ni makutanio ya mifupa miwili katika mwili. Kama wasemavyo wataalamu wa lugha na pia wanaelezea pingili za vidole. Kama hivi Mtume (S.A.W) ameainisha idadi ya vitenganishi vya mwili tokea karne kumi na nne zilizopita na hayo yameoana na hali halisi ya uchunguzi wa mwili wa binadamu. Na kama hivi zinabainika upya dalili za wahyi ambazo hakuna binadamu angeweza kuzijua katika wakati wa Utume.

Tafsili: Kiarabu   

              Kiingereza    Kifaransa     Kijerumani      Kispani      Kituruki       Kiurdu    Kifarsi     Kihausa

Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna   (1428-2007)