|
UKWELI WA KISAYANSI:
Wataalamu wa jiolojia,
wamegundua hivi karibuni kuwa ardhi imegawika kwa wavu
wa mipasuko ya kina katika vipande kumi na mbili vikuu
vinavyopakana ambavyo kila kimoja huitwa bamba (plate)
pamoja na mabamba mengine kadhaa madogo madogo
yanayoitwa vijibamba (platelets). Mabamba hayo huelea
juu ya tabaka ambalo ni kama limeyeyuka. Myeyuko (magma)
huo hupanda baina ya vina vya bahari na huongeza mada
mpya kwenye mabamba mawili yaliyo jirani. Na kwa
kuongezeka upande mmoja, hupungua upande mwengine daima
kwa kuinamia chini ya upande wa bamba jirani. Kama
hivyo, imebainika kuwepo kwa mipasuko mikubwa katikati
ya bahari (Mid-Oceanic Rifts). Mipasuko hiyo huendelea
hadi kuiziba ardhi yote, na kina chake kinaweza kufikia
kilometa 150 kwa mujibu wa kina cha ardhi katika eneo
lenye unene mkubwa zaidi. Pia imebainika kuwa mabara
yote yanayojulikana leo pamoja na kuwa yana milima,
huenda kwa mwendo wa mabamba yanayoyabeba kwa
kukaribiana au kuwa mbali yenyewe kwa yenyewe, mwendo
mdogo kabisa kufikia masafa yasiyopindukia idadi haba ya
sentimeta kila mwaka lakini ni mwendo wenye kuendelea.
Kwa mfano, mwanya wa Bahari ya Sham (Red Sea), unapanuka
kwa sentimeta 3 kila mwaka na mwanya wa ghuba ya
Califonia unaongezeka kwa sentimeta 6 kila mwaka.
Kugongana kwa bamba la India na bamba la jirani yake
baada ya kulika kwa bamba lililo baina yao,
kumesababisha kufanyika kwa msururu wa milima ya
Himalayas ambao una kilima kirefu zaidi duniani.
Inaaminiwa hivi sasa kuwa mabara mapya, yote yalikuwa
ni kitu kimoja kilichoshikamana tokea miaka milioni 200
na kuwa ni bara moja pekee lililo kubwa na bahari moja
yenye kulizunguka lote. Kwa kugawanyika kwake mpasuko wa
asili ukapewa jina la mpasuko wa katikati ya Atlantic
(Mid-Atlantic Ridge) na hadi leo ni eneo la harakati
pevu za volkeno. |
|
UPANDE WA MIUJIZA :
Mipasuko ya katikati
ya bahari (Mid-Ocean Rifts), haikugunduliwa isipokuwa
baada ya vita vya pili vya dunia na imeelezewa kwenye
nadharia ya “ Mabamba ya Tektonic” (Tectonic Plates)
iliyowekwa mwishoni mwa miaka ya sitini na mwanzoni mwa
miaka ya sabini ya karne iliyopita tu. Kwa upande wa
kisayansi, mipasuko hiyo inayoendelea kina chake chini
ya kina cha ardhi, ni alama kubwa zaidi ya gamba la
ardhi. Kwa hiyo Qurani Tukufu inahesabiwa kuwa ndio
iliyotangulia kuashiria uhakika huu uliojificha chini ya
ardhi, na kuwa ni dalili tosha kwamba ni maneno ya
Mwenyezi Mungu Mjuzi Mwenye hekima. |