|
ACHENI KATIKA
MASHUKE YAKE |
Mwenyezi Mungu Mtukufu
Anasema, “ Yussuf! Ewe mkweli ! Tueleze hakika ya
ng’ombe saba wanene kuliwa na ng’ombe saba dhaifu. Na
mashuke saba mabichi na mengine yamekauka, ili nirejee
kwa watu wapate kujua. Akasema: “ Mtalima miaka saba
mfululizo kwa juhudi (yaani limeni miaka saba kwa
juhudi, kwani itaingia njaa kubwa baada ya miaka saba).
Na mtakavyovivuna, viacheni katika mashuke yake,
isipokuwa kidogo mnavyokula (ili mnavyoviacha mule miaka
ya njaa itakayokuja.) Kisha inakuja baadaye miaka saba
ya shida itakayokula vile mlivyoipa (yaani watu watakula
ile akiba mliyoiweka) isipokuwa kidogo mtakachohifadhi
(kwa ajili ya kupandia) |
 |