Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna                          Ukurasa Uliotangulia     Ukurasa Kuu

 

 

 

Hotuba ya Mheshimiwa Dk./ Abdullah bin Abdel Aziz Al-Muslih

Katibu Mkuu wa Bodi ya Kimataifa ya Miujiza ya Kisayansi katika Qurani na Sunna.

 

 

 Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na Mwenye kuneemesha neema ndogo ndogo.

 

Mabibi na mabwana: Wageni wa eneo hili lenye baraka.

     Wafuasi wa miujiza ya kisayansi katika  Qurani na Sunna; ulimwenguni kote. Nakuamkieni kwa maamkizi ya Kiislamu: Assalamu Aleykum wa Rahmatul llahi wa barakatuh. Wabaadu…

Hii leo wameitikia wito wenye shime na miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna duniani toka ulimwenguni kote na wamekutana pembezoni mwa Al Kaabah na chini ya kivuli cha Msikiti Mtukufu wa Makka na wamekusanywa na majengo ya Jumuiya ya dunia ulimwengu wa Kiislamu ili   mkutano huu utoe bodi ya kimataifa ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.

      Hakika ni elimu. Je, hivyo elimu ni nini zaidi ya mwenye kujitolea mhanga mwenyewe.

      Hakika ni yakini. Je, kuna mwenye kuizuia yakini isipokuwa aliyeridhia ujinga kuwa mwenzake.

      Hakika ni muono wa mwenye kuangalia kwa makini dalili  zilipokelewa zilizo thabiti :

      Dalili za kuona na dalili za kuandikwa.

      Dalili katika ulimwengu, binadamu na maisha katika undani wenye kushangaza na katika mpangilio wake katika ufalme huu, mwenye kutasabahi kwa kumshukuru Mola wake.

      Dalili katika kitabu hiki na sunna zimetuzungumzia kuhusu ukweli huu katika maoano kamili na mshikamano mzuri pamoja na kuwa zimeteremka katika wakati ambao haikuwa katika uwezo wa binadamu hata katika elimu yao kuyajua wala kuujua na wala kuuzunguka ukweli huo.

      Hakika ni hoja kubwa yenye kujulisha kuwa aliyeumba ulimwengu ndiye ambaye ameishusha Qurani.

      Hakika risala ya eneo hili la kimataifa ni kutubainishia ukweli huu wenye kung’aa na kuwa ni kivukio cha kuifikia elimu ambayo kwayo tutafikia kumhudumia binadamu katika kutafuta yanayowafaa watu waishi katika ardhi, na tuuthibitishie ulimwengu kuwa dini yetu ni dini ya elimu na maarifa. Inatafuta haki na inalingania kwenye ubunifu, maendeleo na kuchukua sababu ya kuwa juu kimada na kutengeneza ustaarabu kwa ajili ya maisha mazuri ya binadamu yenye uadilifu na elimu kuwa ni kitumishi kwa watu yenye kuwasaidia, na sio tegemezi la kubomoa na sababu ya kuangamiza. Kwa hiyo watu wote watakuwa katika usalama na amani.  (Hakika hii Qurani inaongoza kwa yale ambayo yamenyooka na inawabashiria Waumini wanaofanya mema kuwa wana ujira mkubwa.)

 

      Ama nyinyi wanazuoni, watafiti na watu wa kawaida wa eneo hili la kimataifa!

      Enyi wenye shime ya kushikana na eneo hili ambalo ni kwa ajili yenu na lenu na kutoka kwenu na kwenda kwenu! Ni juu yenu kutoka kwangu na ndugu zangu wanazuoni, watafiti na watu wa uongozi katika bodi ya dunia ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna. Tunashukuru fadhila, na kwa nini isiwe hivyo? Kadhalika mkiwa mashahidi wa Mwenyezi Mungu kwa uungu wake, majina yake, sifa zake na neema zake tukufu  (Ameshuhudia Mwenyezi Mungu kuwa hakuna Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa yeye Mwenyezi Mungu na malaika wake na wenye elimu mwenye kusimamia kwa uadilifu hakuna Mola anayepasa kuabudiwa kwa haki isipokuwa yeye mwenye nguvu na mwenye hekima.)

 

      Bodi hii ambayo ni jumuishi ianayokusanya vigogo wa wanazuoni na wajuzi wa hali ya juu kati ya watafiti katika tafiti za miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna. Katika bodi hii, wanakutana vigogo wa kisayansi wa kimataifa kwa suala hili muhimu kati ya masuala ya dini yetu na sunna za Mtume wetu (S.A.W) kumuita kila mwenye uwezo wa kwenda katika njia hii iliyo sawa na mavuno mazuri kwa ajili ya kuinua haki na kudhihirisha ukweli na kugundua Aliyoyaweka Mwenyezi Mungu katika dunia, na maisha na viumbe, jambo ambalo litafaidisha watu na kufichua neema za Mwenyezi Mungu kwetu ambazo ameziweka katika ufalme wake. ( Yeye ndiye Aliyekuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi ).  ( Sema ewe Muhammad! Angalieni vilivyomo mbinguni na ardhini ).

 

      Bodi ya dunia ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna imejipa jukumu kwa mujibu wa njia ya kisayansi na misingi ya tafiti katika miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna ambayo tunaweza kuyafupisha kama ifuatavyo:

    1- Kuachana na vitu visivyo na vielelezo na nadharia na kukiuka kipindi hiki na kuingia kwenye kipindi cha uhakika wa kisayansi ambacho hakikubali kupingwa wala kubadilishwa.

2.    Kuwepo kwa maana dhahiri juu ya uhakika katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu au Sunna Sahihi za Mtume (S.A.W).

3.     Kuunganisha baina ya uhakika huo na maana ya kifungu kwa mtindo mwepesi na rahisi.

4.  Maana hiyo iwe kwa mujibu wa ufahamu wa Waarabu ambao Qurani imeteremshwa kwa lugha yao.

5.   Kutotafiti katika mambo ya ghaibu ambayo ni Mwenyezi Mungu Pekee ndiye Anayejua elimu yake ambayo tumeyaamini na tumekubali muktadha wake.

6  Tafsiri ya Qurani iwe kwa Qurani, kisha sunna sahihi, kisha kutokana na mambo sahihi yaliyopokelewa toka kwa waliotangulia katika umma huu, kisha kwa maana ya Lugha ya Kiarabu ambayo kwayo imeteremka Qurani Tukufu. 

      Tunapenda kubainisha hapa kuwa shubha ambazo zimezushwa kuhusu tafsiri ya kisayansi – na kadhalika wasiwasi uliotokea katika uwanja wa miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna – ni uhakiki ambao kwa jumla yake uko juu ya tafiti zisizo na mpangilio, kwani wenyewe wameingia katika kuharakisha au kughafilika na baadhi ya misingi iliyowekwa, kwa kujua kuwa tafiti kama hizo si chengine isipokuwa ni hali zisizo za kawaida zenye kukataliwa. Kwa hiyo mazingira ya kimataifa ya miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna wakati unapoangaliwa utafiti kati ya tafiti zinazowekwa kwenye sehemu yake kwa mujibu wa kukurubia kwake kufikia shuruti za tafiti au kuwa kwake mbali na shuruti na misingi hiyo.

      Matatizo ya tafiti katika uwanja huu na uzito tunaoupata, tabu na vikwazo vya uchapishaji, masuala yote hayo athari zake zinaondoka na kupotea vumbi lake wakati tunapoona athari na matunda ya tafiti za miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna. Tunapaswa kutaja baadhi yake kwa ajili ya kuwapa motisha watafiti ili wapite katika njia hii na wainusuru dini ya Mwenyezi Mungu kwayo. Kati ya hayo ni:

1.     Athari kubwa yenye kuachwa katika nyoyo za Waislamu, inayotafsiriwa kwa kuzidi yakini kwao wakati wanapouona uhakika huo na wenye kushangaza, kwani umepokelewa juu ya ulimi wa Mtume asiyejua kusoma wala kuandika Muhammad bin Abdullah (A.S). Kama hivi tunazikuta kuwa ni kihimizo bora cha kushikamana na Qurani na Sunna na kufuata muongozo wao.

2.     Ni jibu la kweli juu ya fikra zenye shaka juu ya usahihi wa risala ya Muhammad, kwani kuuaridhi uhakika huo ulioelezwa na Mtume asiyejua kusoma wala kuandika katika wakati ambao hauna maendeleo ya kisayansi. Pia hakuna katika jamii wala mazingira aliyoishi athari yoyote ya sayansi katika nyanja hizo za kidunia. Kwa hiyo miujiza hii ya kisayansi ni uwanja wenye rutuba kwa ajili ya kuwakinaisha wataalamu waadilifu kuwa Qurani Tukufu inatoka kwa Mwenyezi Mungu na ukweli wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W).

3.     Ni jibu la kisayansi linaloambatana na dalili  ya wazi kuwa dini ya Kiislamu ni kweli dini ya elimu. Kwa himizo la Mtume (SAW)  - na uhimizo wake wa kuitafuta na kudokeza kwake juu ya fadhila za wanazuoni – ametaja hakika nyingi za kisayansi na ameashiria siri nyingi za kidunia juu ya maudhui ya fani nyingi katika upeo wa dunia na hakuna hata mmoja hadi leo anayeweza kuthibitisha kinyume chake, yaani maana za kidunia zilizokuja katika hadithi sahihi pamoja na ukweli wa kisayansi uliofikiwa leo hii.

4.     Miujiza ya kisayansi ni sehemi nzuri kwa Waislamu ili wafuatilizie utafiti, majaribio, kulinganisha na njia nyenginezo za gunduzi za kisayansi na mipango ya kielimu. Wakati huohuo, hayo yanapelekea kupanua duara la miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.

5.     Pia miujiza hii ya kisayansi ni mkondo wa kiusalama unaotoa matawi mengine ya ulinganio wa Mwenyezi Mungu katika ulimwengu wa leo ambao ni ulimwengu wa elimu. Anayefuatilizia sababu za watu wengi kuingia katika Uislamu, ambao walikuwa Wakristo au Mabudha au Mayahudi,  atakuta kuwa baadhi yao wameanza mwendo katika njia ya haki kupitia kuangalia kundi la miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna.

6.     Bila shaka hali ya kurejea kwenye dini ya Uislamu kwa wale ambao wameghafilika, na kama hivi kusilimu kwa wasiokuwa Waislamu,  basi hayo yote yametokana na yakini ya Waislamu kwa dini yao kurejea kwenye hali ya utukufu katika nafsi za vijana wa umma wa Kiislamu baada ya mporomoko uliowapata baada ya kuanguka kwa ukhalifa wa Kiislamu na kuwavaa wasiwasi wa ukoloni.

7.     Haya yote yanatukumbusha ukweli ambao hawendi kinyume hata kidogo na yale aliyotufahamisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (S.A.W) kwa kauli yake: “ Kundi la umma wangu litaendelea kupigania haki wakisaidiana hadi wa mwisho wao apigane na Masihu Dajalu, hawadhuru mwenye kwenda kinyume nao au kutupa mkono hadi itakapokuja amri ya Mwenyezi Mungu.”

         

         Sisi, katika eneo hili la kimataifa, tunatangaza wito mkubwa wa kweli wa kimataifa kwa wanazuoni, watafiti na wenye shime na uwanja wa miujiza ya kisayansi katika Qurani na Sunna washiriki nasi kwa elimu yao, rai zao na nasaha zao. Sisi pamoja na wao, ni washirika katika njia hii. Na kwa ndugu zetu wanaoishi ugenini nje ya ulimwengu wa Kiislamu, tunawapa wito maalumu wa kuwa wawe walinganiaji wa Mwenyezi Mungu katika sehemu hizo kwa kutumia njia hizi za ulinganio zenye kuathiri kwa wenye kufaidika kutoka sehemu hii kutokana na tafiti zilizofikiwa kwa kina. Tunatumai kuwa tutafika pamoja na wote katika tovuti hili hadi iwe ni dira ya tovuti katika uwanja huu na kiini chake.

  

         Wito huu toka sehemu hii ya kimataifa wa kuijaalia anga ya mitandao ya kimataifa ni sehemu ya kukaribisha inayowakusanyeni kwenye meza ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna za Mtume Wake (S.A.W).

         Enyi ndugu! Kuweni askari wa Mwenyezi Mungu katika suala  hili.

                             Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuwafikisha.

 

   Ukurasa Uliotangulia          Ukurasa Kuu