Bodi ya Kimataifa Ya Miujiza Ya Kisayansi Ya Qurani Na sunna    
Risala yetu: Kudhihirisha miujiza ya kisayansi Na kuihakiki na kuichapisha.

Lugha

Ukurasa Uliotangulia

Ukurasa Kuu Falaki Na Anga Ardhi Na Bahari Sheria Za Kiislamu Maneno Mengine  

 

Muhtasari Wa Utafiti Wa Udaktari
Maudhui

Aya Na Hadithi

Kuangalia

SAYANSI  YA  UCHUNGUZI  WA  MWILI  INAAINISHA VITENGANISHI VYA MWILI

Imehadithiwa na Imam Muslim toka kwa Abdullah bin Furukh, amemsikia Aisha akisema kuwa Mtume (S.A.W) amesema, “Kila mtu ameumbwa kutokana na watoto wa Adam kwa viungo mia tatu na sitini. Anayemkabiri Mwenyezi Mungu, akamhimidi Mwenyezi Mungu, akasema La ilaha ila Allah, akamuomba maghfira Mwenyezi Mungu, akaondosha jiwe kwenye njia ya watu au mwiba au mfupa kwenye njia ya watu, na akaamrisha mema au akakataza mabaya kwa viungo hivyo mia tatu na sitini, basi anakwenda siku hiyo hali ya kuwa ameiokoa nafsi yake na moto”.

UTOSI

Mwenyezi Mungu Amesema : “Sivyo hivyo! Kama haachi, Tutamkokota kwa nywele za utosi.  Utosi muongo, wenye madhambi.”  ( Aya za 15-16 Suratul Alaq ).

KUUMWA KWA KIWILIWILI

Mtume (S.A.W) amesema, “ Mfano wa Waumini katika kupendana kwao, kuhurumiana kwao, na kuoneana imani kwao, ni sawa na kiwiliwili. Kikiumwa kiungo kimoja, basi mwili mzima hukesha na kupata homa.”

(Imepokelewa na Bukhari na Muslim na wengineo).

HABA SODA NI DAWA YA KILA UGONJWA

Toka kwa Mtume (S.A.W) amesema, “ Hakuna ugonjwa wowote isipokuwa katika haba soda kuna kupona kwake isipokuwa mauti.”

KIFUPA NDUGU NA MCHIRIZI  WA  ASILI 

Toka kwa Abu Hureira, Mtume (S.A.W) amesema, “ Kila binadamu ataliwa na udongo isipokuwa kifupa ndugu. Kwacho amezaliwa  na ndani yake huumbwa.”

KUUMBWA MTOTO KATIKA MAUMBO TOFAUTI

Mwenyezi Mungu Amesema : “Mmekuwaje hamuweki Heshima ya Mwenyezi Mungu. Na hali ya kuwa Amekuumbeni namna baada ya namna?”. (Aya 13-14 Suratul Nuh).

HISIA  ZA  MAUMIVU 

Mwenyezi Mungu Amesema, “ Hakika wale waliozikataa Aya zetu, Tutawaingiza katika moto. Kila ngozi zao zitakapowiva, Tutawabadilishia ngozi nyengine badala ya zile; ili wawe wanaonja (uchungu wa) adhabu (maisha). Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hekima.” Aya ya 56 ya Suratul Nisaa.
     
     
     
     
     

 

 

 

 

 
 

Kungiyar mu’ujizar ilimi na Alqur’ani da Sunna da duniya  (1428-2007)